Isaiah 3:1-7

Hukumu Juu Ya Yerusalemu Na Yuda.

1 aTazama sasa, Bwana,
Bwana Mwenye Nguvu Zote,
yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda
upatikanaji wa mahitaji na misaada,
upatikanaji wote wa chakula na tegemeo lote la maji,
2 bshujaa na mtu wa vita,
mwamuzi na nabii,
mwaguzi na mzee,
3 cjemadari wa kikosi cha watu hamsini
na mtu mwenye cheo, mshauri,
fundi stadi na mlozi mjanja.

4 dNitawafanya wavulana wawe maafisa wao,
watoto ndio watakaowatawala.
5 eWatu wataoneana wao kwa wao:
mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake.
Kijana atainuka dhidi ya mzee,
mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.

6Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake
katika nyumba ya baba yake na kusema,
“Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu,
tawala lundo hili la magofu!”
7 fLakini siku hiyo atapiga kelele akisema,
“Sina uponyaji.
Sina chakula wala mavazi katika nyumba yangu,
msinifanye niwe kiongozi wa watu.”
Copyright information for SwhNEN